Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » TIMES FM KUTANGAZA MUBASHARA KAGAME CUP
    KITAIFA

    TIMES FM KUTANGAZA MUBASHARA KAGAME CUP

    ChikaoBy ChikaoSeptember 1, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    MSIMU mpya wa Kombe la Kagame (Kagame Cup) unaanza kesho Septemba 2, 2025 kwa mechi mbili kuchezwa kwenye uwanja wa Major General Isamuhyo, Dar es Salaam, mechi hizo zikitarajiwa kutangazwa mubashara na kituo cha radio cha Times FM.

    Times FM imeingia ubia na Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati ( Cecafa) kutangaza mashindano hayo yanayoanza Septemba 2-15 jijini Dar es Salaam.

    Mkuu wa Masoko na mawasiliano wa Cecafa, Andrew Jackson Oryada amesema wameingia ubia na Times FM ambayo itatangaza mubashara mechi zote.

    “Tunafuraha kubwa kuwa mshirika na Times FM, kituo pekee cha radio kinachotangaza michezo hapa nchini Tanzania, tunaamini ushirikiano huu utaongeza kwa kiwango kikubwa mwonekano na usikivu wa Mashindano ya CECAFA Kagame Cup 2025,” alisema.

    Alisema kupitia ushirikiano huo, Times FM itatoa matangazo ya kipekee na ya kina ya mashindano ya Kagame Cup, yakiwemo mahojiano na makocha pamoja na manahodha wa timu, matukio ya nyuma ya pazia wakati wa mazoezi, taarifa kutoka vyumba vya kubadilishia, na maudhui ya mchezaji bora wa mechi.

    Mashindano haya yatashirikisha timu kutoka Tanzania, Zanzibar, Kenya, Rwanda, Burundi, Somalia, Sudan, Sudan Kusini, Djibouti na Ethiopia.

    Mchambuzi wa michezo wa Times FM, Emmanuel Ndalama alisema mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza Septemba 2 hadi 15 yatafuatiliwa moja kwa moja kupitia kituo cha Times FM kama redio mshirika.

    “Wasikilizaji kote nchini Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati wataweza kufuatilia matangazo ya moja kwa moja, mahojiano ya kipekee, uchambuzi wa kina na maoni ya moja kwa moja kutoka viwanjani.

    “Kwa ubia huu, Times FM imeandika historia kama redio pekee ya michezo inayorusha matangazo masaa 24.
    Nyota na nahodha wa zamani wa Yanga, Juma Abdul ambaye ni miongoni mwa wachambuzi wa mashindano hayo kupitia radio ya Times FM alisema ni mashindano ambayo yanakwenda kuongeza ushindani na kuonyesha vipaji vipya, akimtolea mfano nyota wa zamani wa timu hiyo, Didier Kavumbagu ambaye alisajiliwa baada ya kuonekana kwenye Kagame Cup.

    Bingwa wa msimu huu ataondoka na medali ya dhahabu, kombe na kitita cha dola 30,000, mshindi wa pili medali ya fedha na dola 20,000 wakati mshindi wa tatu atapewa dola 10,000 na medali ya shaba.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticlePITIA MAGAZETI YA MICHEZO LEO SEPTEMBA 1, 2025
    Next Article JKT QUEENS WAKABIDHIWA BENDERA KUIWAKILISHA NCHI KIMATAIFA

    Related Posts

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    March 24, 2026

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    March 24, 2026

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    March 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    HII HAPA SABABU KUBWA YA MPANZU KUTO WASALITI SIMBA

    UAMUZI WA KIUFUNDI WAMUWEKA MPANZU SIMBA

    DIARRA AWEKA REKODI, AMUACHA MBALI KIPA WA SIMBA

    Yanga Yamrudisha Kocha Abdihamid Moalin Kuinua Kiwango cha Timu

    Zidane Kurithi Mikoba ya Deschamps Ufaransa Baada ya Kombe la Dunia 2026

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.