Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA
    KITAIFA

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    ChikaoBy ChikaoApril 24, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Bodi ya Ligi Kuu Tanzania imetangaza mabadiliko ya uwanja kwa mchezo wa pili wa Dabi ya Kariakoo msimu wa 2025/26 kati ya Simba na Yanga.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Aprili 24, 2026, mchezo huo sasa utapigwa Mei 03, 2026 saa 12:00 jioni katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, ambao ni uwanja wa nyumbani wa Simba.

    Awali, mchezo huo ulipangwa kufanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, lakini umehamishwa kutokana na uwanja huo kuwa kwenye matengenezo yanayoendelea.

    TPLB imesema imewajulisha rasmi klabu zote mbili, Simba na Yanga, pamoja na wadau wengine wa Ligi Kuu ya NBC kuhusu mabadiliko hayo, na imeeleza kuwa maandalizi ya mchezo yanaanza mara moja ili kuhakikisha unafanyika katika kiwango bora kinachostahili hadhi ya Dabi ya Kariakoo.

    Mchezo huo unatarajiwa kuwa na mvuto mkubwa kutokana na ushindani wa muda mrefu kati ya timu hizo mbili kongwe na zenye mashabiki wengi zaidi nchini Tanzania.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI
    Next Article PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    Related Posts

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    April 25, 2026

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    April 25, 2026

    SIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI

    April 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    SIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.