Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » Refa Aliyeinyima Yanga Penati Afungiwa Mizunguko Mitatu
    KITAIFA

    Refa Aliyeinyima Yanga Penati Afungiwa Mizunguko Mitatu

    ChikaoBy ChikaoMarch 20, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Mwamuzi Ally Mnyupe kutoka Morogoro amefungiwa kuchezesha mechi kwa mizunguko mitatu (3) baada ya kushindwa kutafsiri ipasavyo sheria za mpira wa miguu katika mchezo kati ya Azam FC na Yanga.

    Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa na kumalizika kwa sare tasa, mwamuzi huyo alishindwa kutoa penalti kwa Yanga licha ya tukio la rafu iliyofanywa na beki wa Azam, Fuentes Mendoza, dhidi ya mshambuliaji Prince Dube ndani ya eneo la hatari.

    Kwa mujibu wa Bodi ya Ligi, kupitia Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, mwamuzi huyo alifanya kosa la kiufundi kwa kushindwa kutafsiri sheria za mchezo ipasavyo.

    Mbali na adhabu hiyo, Yanga imetozwa faini ya shilingi milioni tano kutokana na mashabiki wake kuwarushia chupa za maji waamuzi walipokuwa wakitoka uwanjani baada ya kumalizika kwa mchezo huo.

    Aidha, Azam FC nayo imetozwa faini ya shilingi milioni tano kwa kukiuka kanuni za ligi baada ya kukataa kutumia chumba rasmi cha kuvalia na badala yake kutumia njia ya kuingilia vyumbani (corridor) kabla ya kuanza kwa mchezo.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSenegal Wanyang’anywa Ubingwa wa AFCON Kwa Aibu Kubwa! Morocco Washinda Mezani
    Next Article Shabiki wa Yanga Afungiwa Miezi 12 Kwa Uharibifu wa Mali

    Related Posts

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    March 20, 2026

    Refa Aliyeinyima Singida Penati Dhidi ya Simba Afungiwa Mizunguko Mitatu

    March 20, 2026

    Shabiki wa Yanga Afungiwa Miezi 12 Kwa Uharibifu wa Mali

    March 20, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Katibu wa Senegal asema Kombe halitaondoka Nchini kwao.

    FIFA YAPITISHA SHERIA MPYA 6 KUELEKEA KOMBE LA DUNIA 2026

    AUDIO Hanstone Ft Nippi – Usijisumbue DOWNLOAD MP3

    Refa Aliyeinyima Singida Penati Dhidi ya Simba Afungiwa Mizunguko Mitatu

    Shabiki wa Yanga Afungiwa Miezi 12 Kwa Uharibifu wa Mali

    Refa Aliyeinyima Yanga Penati Afungiwa Mizunguko Mitatu

    Senegal Wanyang’anywa Ubingwa wa AFCON Kwa Aibu Kubwa! Morocco Washinda Mezani

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.