Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema timu hiyo itawakosa baadhi ya nyota wake muhimu katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Namungo FC utakaopigwa leo Aprili 19, 2026, kwenye Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Wachezaji watakaokosekana ni beki wa kushoto Nickson Kibabage ambaye anaendelea kuuguza majeraha, pamoja na kiungo Alassane Kante anayekosa mchezo huo kutokana na adhabu ya kadi nne za njano.
Pamoja na changamoto hiyo, Matumaini bado ni makubwa baada ya kurejea kwa Shomari Kapombe na Yusuph Kagoma, ambao wanatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachoshuka dimbani dhidi ya Namungo FC.
