Hadi sasa msimu ukiendelea kushika kasi, mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu katika Ligi Kuu ya NBC zimezidi kuwa kali na zenye ushindani mkubwa. Mshambuliaji Selemani Mwalimu ameendelea kuwa moto, akifikisha jumla ya mabao sita (6) na kujipanga sambamba na washambuliaji wengine hatari kama Prince Dube, Depu na Saleh Karabaka kwenye orodha ya wafungaji bora.
Kinara wa ufungaji kwa sasa ni Fabrice Ngoy mwenye mabao nane (8), akifuatiwa kwa karibu na Feisal Salum ‘Fei Toto’ aliyefunga mabao saba (7). Hali hii inaonyesha wazi namna ushindani ulivyo mkali, huku Mwalimu akithibitisha ubora wake mbele ya lango na kuendelea kuwa miongoni mwa washambuliaji wanaotikisa ligi.
Kwa upande wa pasi za mabao (assists), Feisal Salum na Elie Mpanzu ndio wanaoongoza, kila mmoja akiwa na pasi tano (5). Takwimu hizi zinaonyesha kuwa msimu huu si tu wa ushindani wa ufungaji, bali pia ubunifu wa kutengeneza nafasi, hali inayoongeza mvuto mkubwa katika mbio za ubingwa pamoja na tuzo za wachezaji binafsi.
