Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » DURU LA PILI MOTO, DEPU ARUDI, YANGA YAANZA VITA RASMI
    KITAIFA

    DURU LA PILI MOTO, DEPU ARUDI, YANGA YAANZA VITA RASMI

    ChikaoBy ChikaoApril 3, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KUREJEA kwa mshambuliaji wa Yanga, Laurindo Dilson Maria Aurélio ‘Depu’, kumekipa kikosi hicho nguvu mpya na kuibua matumaini makubwa kuelekea duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara.

    Nyota huyo alikuwa akisumbuliwa na majeraha yaliyomuweka nje katika baadhi ya mechi za mwisho za mzunguko wa kwanza, hali iliyopunguza makali ya safu ya ushambuliaji ya timu hiyo.

    Hata hivyo, sasa Depu amepona na kurejea rasmi kikosini, jambo ambalo limeongeza chachu ndani ya timu huku wachezaji na benchi la ufundi wakionekana kuwa na morali ya juu.

    Akizungumza kuhusu hali ya kikosi, Msemaji wa Yanga, Ali Kamwe, amesema kurejea kwa wachezaji waliokuwa majeruhi, akiwemo Depu, ni ishara njema kwa timu yao kuelekea hatua inayofuata ya ligi.

    “Ligi irudi sasa, tumetimia. Wachezaji wetu waliokuwa majeruhi wamerejea na tayari wameanza mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu,” amesema Kamwe.

    Yanga tayari imeanza mazoezi makali ikijiandaa na mchezo wao wa kwanza baada ya mapumziko ya FIFA Series, wakilenga kuanza kwa ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri ya ushindani.

    Katika mchezo huo, Yanga inatarajiwa kukutana na Tanzania Prisons, Jumamosi, Aprili 4, 2026, kwenye Uwanja wa KMC Complex, Mwenge jijini Dar es Salaam, huku macho na masikio ya mashabiki yakielekezwa kuona kiwango cha Depu baada ya kurejea dimbani.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSURE BOY AOMBA KUONDOKA YANGA
    Next Article BACCA ATUPA TAULO, AKIRI RUSHINE NI BALAA

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.