HomeKITAIFAYANGA YATANGAZA VITA, PRESHA YAHAMIA ZANZIBAR

YANGA YATANGAZA VITA, PRESHA YAHAMIA ZANZIBAR

KUELEKEA mchezo wa kesho wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya JS Kabylie, Kocha Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves amesema kikosi chake kipo tayari kwa mapambano makali dhidi ya wapinzani hao wanaoheshimika barani Afrika.

Akizungumza kuelekea mchezo huo muhimu wa hatua ya makundi utakaochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex,Pedro amesema JS Kabylie ni timu imara yenye uzoefu mkubwa, hasa katika michuano ya kimataifa.

Amebainisha kuwa wapinzani wao wamewekeza kwa kiasi kikubwa msimu huu wakilenga kurejea katika historia yao ya mafanikio.

Kocha huyo ameweka wazi kuwa maandalizi ya Yanga yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha, huku benchi la ufundi likifanya uchambuzi wa kina kuhusu ubora na mapungufu ya wapinzani wao.

“Tunawafahamu vizuri. Tumechambua namna wanavyocheza na tumejiandaa kukabiliana nao kwa umakini mkubwa,” amesisitiza.

Pedro aliongeza kuwa licha ya JS Kabylie tayari kutokuwa na presha ya kufuzu, bado watashuka dimbani kupigania heshima ya klabu yao.

“Wanakuja bila presha kwa sababu tayari wameshatoka kwenye mashindano, lakini hilo linaweza kuwafanya wacheze kwa uhuru zaidi. Hivyo ni lazima tuwe makini kwa dakika zote 90,” amesema.

Ameongeza  kuwa huu ni muda wa Yanga kuonyesha ubora wao na kupigania nafasi ya kusonga mbele, mechi hiyo kuwa ngumu, umuhimu wa nidhamu, umakini na kutumia vyema nafasi zitakazopatikana.

Kwa sasa msimamo wa Kundi B unaongozwa na Al Ahly SC wenye pointi tisa, wakifuatiwa na AS FAR Rabat wenye pointi nane. Yanga wanashika nafasi ya tatu wakiwa na pointi tano, huku JS Kabylie wakiburuza mkia kwa pointi tatu.

Pedro anaamini kikosi chake kiko tayari kufanya hesabu sahihi na kupambana hadi mwisho, akitumaini kupata pointi muhimu zitakazowaweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua inayofuata ya mashindano hayo.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Most Popular