Home KITAIFA SIMBA YALENGA DODOMA, DERBY SIO KIPAUMBELE

SIMBA YALENGA DODOMA, DERBY SIO KIPAUMBELE

0
26

SIMBA SC imeweka wazi kuwa kwa sasa fikra zake ziko kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Dodoma Jiji FC, huku Kariakoo Derby dhidi ya Yanga SC ikiwa bado ni suala la baadaye.

Beki wa Simba, David Kamenta “Duchu”, amesema  kuwa kikosi chake kitapambana kwa nguvu zote katika mchezo wa Dodoma ili kukamilisha kampeni yao ya kupata alama sita katika michezo miwili mfululizo.

“Tutakamilisha kampeni yetu ya kupata alama sita, tatu tayari tumepata, bado tatu za Dodoma ziko mbele yetu. Baada ya mechi hiyo, tutakaa chini na kuanza kupanga mikakati ya Kariakoo Derby,”  amesema Duchu.

Simba itashuka dimbani kesho kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, kwa lengo la kuhakikisha wanapata alama tatu muhimu mbele ya wenyeji wao.

Beki huyo ameongeza kuwa malengo ya timu ni kuhakikisha kila tone la jasho linatumika vizuri, ili kuimarisha heshima ya klabu ndani ya ligi na katika michuano ya kimataifa.

“Kwa sasa, tunalenga mchezo huu na nguvu zetu zote. Baada ya Dodoma, ndio tutafikiria Kariakoo Derby,” Duchu amesema, akisisitiza umuhimu wa kuzingatia kila hatua kwa kila mchezo.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here