Home KITAIFA ONYO LA MAPEMA, YANGA YAREJEA KILELENI KWA KISHINDO

ONYO LA MAPEMA, YANGA YAREJEA KILELENI KWA KISHINDO

0
31

KLABU  ya Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo uliopigwa kwa ushindani mkubwa.l katika dimba la KMC Complex uliopo Mwenge Dar es Salaam.

Katika pambano hilo, Yanga ilionyesha ubora mkubwa kuanzia dakika za mwanzo hadi mwisho wa mchezo, ikitawala umiliki wa mpira na kutengeneza nafasi nyingi za mabao.

Ushindi huo umeipa timu hiyo morali kubwa kuelekea michezo ijayo, hususan Kariakoo Derby inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki.

Mabao ya Yanga yalifungwa na Mohamed Hussein, Laurindo Dilson ‘Depu’, Mudathir Yahya, Prince Dube na Sheikhan Khamis, kila mmoja akichangia kwa namna yake kuifanya timu hiyo iondoke na alama zote tatu muhimu.

Kwa matokeo hayo, Yanga imefikisha pointi 28 na kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi sawa na JKT Tanzania waliopo nafasi ya pili. Hata hivyo, Yanga inaongoza kutokana na ubora wa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Ushindi huo si tu umeimarisha nafasi yao juu ya msimamo, bali pia umetuma salamu nzito kwa wapinzani wao kabla ya Kariakoo Derby, huku kikosi hicho kikionekana kuwa katika kiwango bora na tayari kwa mapambano makubwa yanayofuata.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here