Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » CAF IMEISHA SASA TUNAREJESHA HESHIMA LIGI KUU
    KITAIFA

    CAF IMEISHA SASA TUNAREJESHA HESHIMA LIGI KUU

    ChikaoBy ChikaoFebruary 16, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    BAADA kuondolewa  katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, ameweka wazi malengo yake mapya akiwataka wachezaji wake kuhamishia nguvu zote kwenye mashindano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

    Barker aliyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa dakika 90 za mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Stade Malien, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa  jijini Dar es Salaam.

    Licha ya ushindi huo, matokeo ya jumla hayakutosha kuiwezesha Simba kusonga mbele, jambo lililowafanya kuaga rasmi mashindano hayo.

    Barker amesema amefurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake, akisisitiza kuwa ameona mabadiliko chanya na ukuaji mkubwa wa kikosi chake kadri mashindano yalivyokuwa yakiendelea.

    Kocha huyo ameeleza  kuwa sasa ni wakati wa kuangalia mbele na kujipanga upya kwa ajili ya malengo yaliyosalia ndani ya msimu huu, kuwa Ligi Kuu Tanzania Bara ni fursa muhimu kwa timu hiyo kurejesha heshima na kuonyesha ubora wao.

    “Tumeondolewa kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini bado tuna Ligi Kuu Tanzania Bara. Tunakwenda kujiandaa vizuri na kupambana kutafuta matokeo chanya katika kila mechi,” amesema Barker.

    Ameongeza  kuwa dhamira yao ni kuhakikisha wanamaliza msimu wakiwa katika nafasi nzuri itakayowapa nafasi ya kushiriki tena Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao, akiamini kuwa uzoefu walioupata msimu huu utakuwa chachu ya mafanikio yajayo.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleVideo Mpya ya G Nako Inakumbusha Mashabiki Burudani ya Bongo Fleva
    Next Article UKWELI KUHUSU ISHU YA PENATI YA NAMUNGO

    Related Posts

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    April 12, 2026

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    April 8, 2026

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    April 8, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    MPANZU NA FEI TOTO WAKUTANA USO KWA USO KWENYE VITA YA ASSIST

    IBENGE ATANGAZA VITA JUU YA KIKOSI CHA SIMBA

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.