Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » VINARA LIGI DARAJA LA KWANZA RAHA TUPU
    KITAIFA

    VINARA LIGI DARAJA LA KWANZA RAHA TUPU

    ChikaoBy ChikaoMarch 15, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    VINARA wa Ligi Daraja la kwanza Kanda ya Unguja, Black Sailors, wamesema msimamo umekuwa hamasa nzuri ya kuanza mazoezi kwa ari zaidi.

    Kauli hiyo imetolewa na Kocha Msaidizi, Said Mwinyi akisema amefurahishwa na namna wachezaji walivyoanza mazoezi kwa ari kubwa.

    Black Sailor inaongoza ligi hiyo kwa pointi 53 ilizovuna katika mechi 20 na kubakisha mechi 10 kukamilisha msimu wa 2025-2026.

    “Wachezaji wanaendelea kuonyesha kiwango kizuri na utimamu wa mwili tangu walivyorejea mazoezini kutoka mapumziko mafupi kwa ajili ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, hali inayotupa matumaini makubwa benchi la ufundi kuelekea michezo iliyobaki,” amesema.

    Amesema sio kawaida kwa timu kuanza mazoezi kwa ari kubwa kwani hawakuonekana kama walikuwa wametoka katika mapumziko akibainisha jambo hilo linaashiria wengi wao waliendelea kufanya mazoezi binafsi wakati wa kipindi chote cha mapumziko.

    “Mazoezi yanaendelea vizuri na wachezaji wanaonesha kujituma kwa kiwango kikubwa, hali yao ya mwili ni nzuri na inaonekana walikuwa wanafanya mazoezi binafsi hata wakati wa mapumziko,” alisema Mwinyi.

    Baada ya ligi hiyo kurejea, Black Sailors mchezo wake wa kwanza itacheza Machi 30, 2026 dhidi ya Sebleni United, kisha Aprili 6, dhidi ya ZAFSA. Kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo, timu mbili za juu katika msimamo wa ligi zitapanda daraja kucheza Ligi Kuu Zanzibar, wakati timu nne za mwisho zikishuka daraja la pili Mkoa. Ligi hiyo ina timu 16.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous Article“Reece James ni beki bora zaidi wa kulia Duniani”-Rosenior.
    Next Article MAJERUHI YATIKISA SIMBA, NANGU KURUDI JULAI

    Related Posts

    MAJERUHI YATIKISA SIMBA, NANGU KURUDI JULAI

    March 15, 2026

    BAJABER ARUDI KWENYE RAMANI KUPITIA WITO WA TAIFA

    March 15, 2026

    YANGA WAINGIA UWANJA WA MKAPA WAKIWA NA MIKAKATI YA KUIFUNGA AZAM FC

    March 15, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    MAJERUHI YATIKISA SIMBA, NANGU KURUDI JULAI

    VINARA LIGI DARAJA LA KWANZA RAHA TUPU

    “Reece James ni beki bora zaidi wa kulia Duniani”-Rosenior.

    BAJABER ARUDI KWENYE RAMANI KUPITIA WITO WA TAIFA

    YANGA WAINGIA UWANJA WA MKAPA WAKIWA NA MIKAKATI YA KUIFUNGA AZAM FC

    Tanzania Yatoa Zaidi ya Sh80 Bilioni CAF Ili Kuwa Mwenyeji wa AFCON 2027

    Bilioni Zatengwa 388.8 Kujenga AFCON City Unguja

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.