“Simba na Yanga haziwezi kuachana kushindana na kutaniana, na huo ndio utani wa jadi wenyewe, mmoja anapofanya vizuri lazima atamtambia asifanya vizuri, kila timu inatamba kwa wakati wake, ingawa ninachokisisitiza utani wa jadi siyo ugomvi wala uadui,” anasema Kibadeni.
Kocha wa JKT Tanzania, Ahmad Ally anasema: “Tuzo zinawapa motisha wachezaji kuongeza bidii kuona mchango wao unatambuliwa zaidi uwanjani, hicho ni kitu kizuri zaidi.”
Beki wa zamani wa Yanga, Oscar Joshua anasema: “Kuna hisia ya furaha mchezaji anaipata anapopewa tuzo ya kutambuliwa kufanya vizuri katika mechi, inamuongezea morali ya kupambana kwa lengo la kuchukua zaidi na zaidi.”
Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Shaban Kisiga anasema: “Tuzo ni heshima kwa mchezaji, ukiacha tu ile ya kila mechi zipo nyingi, hilo linampa nguvu mchezaji na kujiona anathaminiwa, kuhusu Simba na Yanga zina ushindani ambao hauwezi kuisha.”
WASIKIE MASTAA SIMBA, YANGA
Kwa upande wa Gueye, anasema: “Ushindani wa Ligi Kuu Tanzania ni mgumu, jambo la msingi ni kupambania ubingwa, lakini nafurahi kuchukua tuzo hizo.”
Vivyo hivyo kwa Rushine anasema anashukuru kwa sapoti wanayoipata kutoka kwa mashabiki wao, hao ndio wanawapa nguvu ya mapambano, huku akibainisha kwamba, kubwa zaidi anatamani kuona Simba inahukua ubingwa.
Kwa upande wa kipa wa Yanga, Diarra anasema: “Nina furaha, nashukuru mashabiki wanaotusapoti, tutapata moyo wa kupambana.”