Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » UWANJA WA MKAPA KUFUNGWA KUPISHA AFCON 2027
    KITAIFA

    UWANJA WA MKAPA KUFUNGWA KUPISHA AFCON 2027

    ChikaoBy ChikaoMarch 3, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    SERIKALI imetangaza kuufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia mwezi huu ili kupisha awamu ya mwisho ya ukarabati mkubwa, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027.

    Akizungumza katika mahojiano na gazeti la The Citizen, Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amethibitisha kuwa ukarabati huo utachukua kati ya miezi sita hadi mwaka mmoja.

    Msigwa amebainisha kuwa, awamu hii ya mwisho itahusisha maboresho makubwa kwenye eneo la kuchezea (pitch) na maeneo mengine muhimu ya uwanja huo ili kukidhi vigezo vya kimataifa.“Huu ni ukarabati wa mwisho ambao utahusisha kazi kubwa kwenye nyasi na miundombinu inayozunguka uwanja. Pindi kazi itakapoanza, uwanja hautatumika kwa mechi yoyote,” amesema Msigwa.

    Aidha, aliongeza kuwa iwapo kuna ratiba za mechi zinazoweza kukamilika kabla ya ukarabati kuanza, mechi hizo zitaendelea kama zilivyopangwa. Hata hivyo, alisisitiza kuwa timu zinazoutumia uwanja huo zitalazimika kutafuta viwanja mbadala mara tu kazi itakapoanza.

    Kwa mujibu wa maboresho ya ratiba ya Ligi Kuu Bara, mechi tatu kwa msimu huu zimepangwa kuchezwa hapo ambazo ni Azam vs Yanga (Machi 15, 2026), Azam vs Simba (Aprili 5, 2026) na Simba vs Yanga (Mei 1, 2026).

    Hatua hii ya kuufunga uwanja huo inatarajiwa kuwa na athari kubwa kwa soka la ndani na kimataifa, ikizingatiwa kuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa ndio kitovu kikuu cha mechi kubwa na za kitaifa nchini Tanzania.Source, The Citizen

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMSHAMBULIAJI MTANZANIA ASIMULIA ATHARI IRAN
    Next Article SOWAH APELEKWA KAMATI YA NIDHAMU SIMBA SC

    Related Posts

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    April 26, 2026

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    April 25, 2026

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    April 25, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.