Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » UWANJA WA MKAPA KUFUNGWA KUPISHA AFCON 2027
    KITAIFA

    UWANJA WA MKAPA KUFUNGWA KUPISHA AFCON 2027

    ChikaoBy ChikaoMarch 3, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    SERIKALI imetangaza kuufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa kuanzia mwezi huu ili kupisha awamu ya mwisho ya ukarabati mkubwa, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027.

    Akizungumza katika mahojiano na gazeti la The Citizen, Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amethibitisha kuwa ukarabati huo utachukua kati ya miezi sita hadi mwaka mmoja.

    Msigwa amebainisha kuwa, awamu hii ya mwisho itahusisha maboresho makubwa kwenye eneo la kuchezea (pitch) na maeneo mengine muhimu ya uwanja huo ili kukidhi vigezo vya kimataifa.“Huu ni ukarabati wa mwisho ambao utahusisha kazi kubwa kwenye nyasi na miundombinu inayozunguka uwanja. Pindi kazi itakapoanza, uwanja hautatumika kwa mechi yoyote,” amesema Msigwa.

    Aidha, aliongeza kuwa iwapo kuna ratiba za mechi zinazoweza kukamilika kabla ya ukarabati kuanza, mechi hizo zitaendelea kama zilivyopangwa. Hata hivyo, alisisitiza kuwa timu zinazoutumia uwanja huo zitalazimika kutafuta viwanja mbadala mara tu kazi itakapoanza.

    Kwa mujibu wa maboresho ya ratiba ya Ligi Kuu Bara, mechi tatu kwa msimu huu zimepangwa kuchezwa hapo ambazo ni Azam vs Yanga (Machi 15, 2026), Azam vs Simba (Aprili 5, 2026) na Simba vs Yanga (Mei 1, 2026).

    Hatua hii ya kuufunga uwanja huo inatarajiwa kuwa na athari kubwa kwa soka la ndani na kimataifa, ikizingatiwa kuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa ndio kitovu kikuu cha mechi kubwa na za kitaifa nchini Tanzania.Source, The Citizen

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMSHAMBULIAJI MTANZANIA ASIMULIA ATHARI IRAN
    Next Article SOWAH APELEKWA KAMATI YA NIDHAMU SIMBA SC

    Related Posts

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    April 12, 2026

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    April 8, 2026

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    April 8, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    MPANZU NA FEI TOTO WAKUTANA USO KWA USO KWENYE VITA YA ASSIST

    IBENGE ATANGAZA VITA JUU YA KIKOSI CHA SIMBA

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.