Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » BEI MBAYA AKIRI SIMBA IMEMFUNDISHA SOMO ZITO
    KITAIFA

    BEI MBAYA AKIRI SIMBA IMEMFUNDISHA SOMO ZITO

    ChikaoBy ChikaoMarch 8, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KOCHA Mkuu wa timu ya B19 maarufu kama Mabeberu wa Jiji, Twaha Beimbaya amesema mchezo wao dhidi ya Simba SC umekuwa somo kubwa kwa kikosi chake, akieleza kuwa vijana wake wamepata uzoefu mkubwa licha ya kuondolewa katika hatua ya 32 ya Kombe la Shirikisho la CRDB.

    Katika mchezo huo uliochezwa jana usiku kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni, Dar es Salaam, B19 walilazimika kuaga mashindano hayo baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Simba, matokeo yaliyothibitisha ubora wa wapinzani wao katika mechi hiyo.

    Beimbaya amesema kuwa pamoja na matokeo hayo, kikosi chake kilijitahidi kupambana kadiri kilivyoweza, lakini uzoefu mkubwa wa wachezaji wa Simba uliwapa faida kubwa katika kutumia makosa yaliyojitokeza upande wa wapinzani wao.

    Ameongeza kuwa bao la kwanza walilofungwa lilitokana na uzembe wa mchezaji mmoja mmoja, hali iliyowapa Simba nafasi ya kujiamini zaidi na kuendeleza presha ambayo hatimaye iliwawezesha kupata ushindi huo.

    Kocha huyo amesema kabla ya mchezo aliwapa maelekezo maalum wachezaji wake ili waweze kucheza kwa nidhamu na kufuata mbinu walizopanga, na kwa kiasi kikubwa walijitahidi kuyatekeleza licha ya kukutana na upinzani mkali.

    “Simba ni timu kubwa, niliwapa maelekezo vijana wangu na kwa kiasi fulani walijitahidi kuyafuata, lakini kutokana na uzoefu na ubora wa mpinzani wetu waliweza kutumia makosa yetu na kupata ushindi,” alisema Beimbaya.

    Amesisitiza kuwa wanachokichukua kutoka katika mchezo huo ni uzoefu na mafunzo muhimu yatakayowasaidia katika michezo ya Championship, akiamini kuwa wakifanyia kazi makosa yao wana nafasi nzuri ya kurejea tena katika Kombe la Shirikisho la CRDB msimu ujao na kufanya vizuri zaidi.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSOWAH APELEKWA KAMATI YA NIDHAMU SIMBA SC
    Next Article SIMBA WATUMA SALAMU KALI, JINA LA MPINZANI HALINA MAANA

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.