Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA WATUMA SALAMU KALI, JINA LA MPINZANI HALINA MAANA
    KITAIFA

    SIMBA WATUMA SALAMU KALI, JINA LA MPINZANI HALINA MAANA

    ChikaoBy ChikaoMarch 8, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KIUNGO wa Simba SC, Innocent Loemba amesema kwa sasa kikosi chao hakitazami majina ya wapinzani wanaokutana nao, bali kimeweka nguvu zote katika kusaka ushindi na alama tatu muhimu katika kila mchezo wanaocheza.

    Nyota huyo ameeleza kuwa ushindani ndani ya ligi umekuwa mkubwa kwa kila timu, hali inayowalazimu wachezaji wa Simba kuingia uwanjani wakiwa na ari kubwa ya kupambana ili kuhakikisha wanaitetea nembo ya klabu yao kwa nguvu zote.

    Loemba amesema kuwa kwa sasa wachezaji wamekubaliana kuweka pembeni majina makubwa au madogo ya wapinzani wao, kwa sababu wanatambua kuwa kila timu inayokutana nao inakuwa na malengo yake ya kupata matokeo mazuri.

    Amesisitiza kuwa kila mchezo kwao ni muhimu na haupaswi kubezwa, kwani timu nyingi zimekuwa zikionyesha ushindani mkubwa pindi zinapokutana na Simba, jambo linalowafanya wao kuongeza umakini zaidi ndani ya uwanja.

    “Hakuna mechi iliyorahisi kwetu, hatuangalii timu tunakutana nayo iwe Singida Black Stars au Pamba Jiji FC, kikubwa ni kuingia kwa nguvu, mshikamano na kupambana kutafuta alama tatu ili kufikia malengo yetu,” amesema Loemba.

    Kiungo huyo ameweka wazi kuwa ushindani uliopo ndani ya kikosi cha Simba kwa sasa ni mkubwa, jambo linalowafanya wachezaji kujituma zaidi kila wanapopata nafasi ya kucheza ili kusaidia timu kupata matokeo chanya.

    Loemba ameongeza kuwa nguvu kubwa wanayoipata inatokana na mashabiki wa Simba ambao wamekuwa wakiisapoti timu hiyo kila wanapocheza, jambo linalowapa hamasa wachezaji kupambana zaidi ili kuendelea kuwapa furaha mashabiki hao kila wanapopata nafasi ya kushuka dimbani.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleBEI MBAYA AKIRI SIMBA IMEMFUNDISHA SOMO ZITO
    Next Article MAJERUHI YAWALAZIMISHA PEDRO KUBADILI KIKOSI YANGA

    Related Posts

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    April 26, 2026

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    April 25, 2026

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    April 25, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.