Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » Aziz Ki aandika ujumbe mzito kwa Hamisa Mobetto siku yake ya kuzaliwa.
    KITAIFA

    Aziz Ki aandika ujumbe mzito kwa Hamisa Mobetto siku yake ya kuzaliwa.

    ChikaoBy ChikaoDecember 11, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Mchezaji wa zamani wa Yanga anayekipiga klabu ya Wydad kwa sasa Stephane Aziz Ki ameandika ujumbe mzito kwenye ukurasa wake wa Instagram akimtakia kila la kheri mke wake mwanamitindo wa Tanzania Hamisa Mobetto katika kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa.

    Aziz Ki ambaye alifunga ndoa na mwanamitindo huyo wa Tanzania mapema mwaka huu kwa sasa anakipiga Nchini Morocco huku mpaka sasa wakiwa bado hawajajaliwa kupata mtoto pamoj licha ya kila mmoja kuwa na watoto nje ya ndoa yao.

    “Mpenzi wangu Hamisamobetto,
    Katika siku hii maalum, nataka nikukumbushe umuhimu wako maishani mwangu. Kila mwaka nikiwa pembeni yako ni zawadi ya thamani—sura mpya iliyojaa mapenzi, furaha, na kumbukumbu zisizosahaulika.

    Wewe ni nguvu yangu, upole wangu, amani yangu, na msukumo wangu. Kwa sababu yako mimi ni mwanaume bora, na kila muda ninaokuona hunikumbusha jinsi nilivyo barikiwa kukupenda na kupendwa na wewe.

    Leo, siadhimishii tu siku yako ya kuzaliwa… ninaadhimisha mwanamke wa kipekee uliye: moyo wako mkarimu, tabasamu lako la faraja, ujasiri wako, nuru yako, na namna uwepo wako unavyoangaza maisha yangu.

    Naomba mwaka huu mpya wa maisha yako uje na furaha zaidi, mafanikio, amani, na upendo. Na ujue kwamba daima nitakuwa hapa kando yako—kukupenda, kukusaidia, na kukuthamini jinsi unavyostahili.

    Heri ya Siku ya Kuzaliwa, malkia wangu.

    Nakupenda zaidi ya maneno yanavyoweza kuelezea,
    MIRS KI”Ameandika Azizi Ki.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleDavies arejea uwanjani baada ya kuuguza goti kwa siku 262
    Next Article Chico Ushindi Afariki, Soka la Afrika Lapata Pengo

    Related Posts

    Mshindi lazima apatikane leo Yanga SC vs Simba SC, Muungano CUP

    April 29, 2026

    IBENGE AKIRI KUTORIDHISHWA NA KIWANGO CHA WACHEZAJI WAKE

    April 26, 2026

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    April 26, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Wafungaji Bora Mapinduzi Cup 2026

    Mshindi lazima apatikane leo Yanga SC vs Simba SC, Muungano CUP

    IBENGE AKIRI KUTORIDHISHWA NA KIWANGO CHA WACHEZAJI WAKE

    matokeo ya Azam FC vs Yanga SC Leo 25/04/2026

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.