Mshindi lazima apatikane leo Yanga SC vs Simba SC, Muungano CUP leo Aprili 29, 2026 Uwanja wa New Amaan Complex.
Mchezo huu unatarajiwa kuchezwa saa 2:15 kwa wababe hawa kusaka mshindi wa taji hilo ambalo lipo mikononi mwa Yanga SC.
Yanga SC chini ya Kocha Mkuu, Pedro Goncalves anatarajia kupambana na Simba SC inayonolewa na Kocha Mkuu, Steve Berkar.
Pedro ameweka wazi kwamba wanahitaji ushindi kwenye mchezo wa leo kwa kuwa wamefanya maandalizi mazuri kuelekea mchezo wa leo.
“Tupo tayari kwa mchezo na maandalizi yamekamilika kikubwa ni kuona tunapata matokeo mazuri kwa kuwa tulikuwa na malengo mwanzo wa msimu na tunaendelea kupambana,”.
Seleman Matola, kocha msaidizi wa Simba SC, amesema wanatambua ni mchezo wa fainali utakuwa na ugumu hivyo watapambana kupata matokeo.
