Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » “Xavi ameumia wachezaji wale wale Hans Flick anashinda”Laporta.
    KIMATAIFA

    “Xavi ameumia wachezaji wale wale Hans Flick anashinda”Laporta.

    ChikaoBy ChikaoMarch 10, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Mgombea urais wa Barcelona, Joan Laporta, amefunguka kuhusu kauli zilizotolewa na Xavi Hernández katika mahojiano yake na La Vanguardia akisema Xavi anaumizwa na mafanikio ya Hans Flick anayoyapata akiwa na wachezaji wale wale aliokuwa nao Xavi.

    Kiungo huyo wa zamani na kocha aliushambulia vikali uongozi wa zamani, akimlaumu Laporta kwa kushindikana kurejea kwa Lionel Messi mwaka 2023, huku pia akidai kuwa mshirika wa karibu wa Laporta, Alejandro Echevarria, ndiye anayeendesha mambo ndani ya klabu.

    Laporta ameweka wazi kuwa ameumizwa na kauli za Xavi na akasisitiza kuwa uamuzi wake wa kuachana na kocha huyo wa zamani ulikuwa sahihi.

    “Nilishangaa na kuumia. Ninapoona kauli hizi kutoka kwa Xavi, namfikiria Hansi Flick. Ni vigumu kuwa rais wa Barça na lazima uchukue maamuzi magumu nilifanya kile nilichopaswa kufanya,”

    “Kwa Xavi, niliona kwamba tulikuwa tunaenda kupoteza, na kwa Flick ninaona kwamba tutaenda kushinda ninaelewa kwamba ameumia kwa wachezaji wale wale, Xavi alikuwa anapoteza, na Flick anashinda.”

    “Haya ni maamuzi matatu magumu zaidi niliyowahi kufanya: Lionel Messi, Ronald Koeman na Xavi Hernández. Niliyafanya nikiweka maslahi ya Barça mbele. Wawili kati yao nilikuwa nao kama wachezaji, lakini haya ni maamuzi ambayo lazima yafanywe. Wote ni magwiji wa Barça”.

    “Barça haiwezi kuendeshwa kwa kutumia kompyuta tu; ni suala la hisia. Barça iko juu ya wachezaji na hata marais.” Amesema Laporta.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleKAGOMA ASEMA BADO ANA KAZI KUBWA SIMBA
    Next Article Barcelona Inaweza Kuwa na Kipaumbele Kumchukua Erling Haaland

    Related Posts

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    April 25, 2026

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    April 25, 2026

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    April 17, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    SIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.