Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » Hawaongozi Ligi, Ni Wamecheza tu Mechi Nyingi
    KITAIFA

    Hawaongozi Ligi, Ni Wamecheza tu Mechi Nyingi

    ChikaoBy ChikaoNovember 13, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    AHMED Ally, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba SC, ameweka wazi kuwa tofauti ya pointi kwenye msimamo wa ligi inasababishwa na idadi ya mechi ambazo timu zimecheza.

    Kwa mujibu wa mwenendo wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2025/26, vinara kwa sasa ni Yanga SC inayoongozwa na Kocha Pedro Gonçalves, ikiwa imecheza michezo minne na kujikusanyia pointi 10.

    Simba SC inashika nafasi ya pili, ikiwa imeshuka dimbani mara tatu pekee sawa na dakika 270, na imekusanya jumla ya pointi 9.

    Mchezo wao wa mwisho kabla ya ligi kusimama ulikuwa dhidi ya JKT Tanzania ugenini, ambapo Simba ilipata ushindi wa 2-1. Katika mchezo huo, bao la JKT lilifungwa na Edward Songo, huku mabao ya Simba yakifumwa kimiani na Wilson Nangu pamoja na Jonathan Sowah.

    Akizungumzia hali ilivyo kwenye msimamo, Ahmed Ally alisema:

    “Msimu huu tumejitahidi sana kutafuta matokeo kwenye kila mchezo. Ikiwa unaona timu fulani inaongoza kwa sasa, ni kwa sababu imetushinda kwenye idadi ya mechi ilizocheza. Lakini upande wa matokeo tumeonyesha uimara mkubwa.”

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMukwala Mambo Bado Magumu Simba, Shida Nini!!?
    Next Article Kocha wa Mamelodi Ageukia Uchungaji

    Related Posts

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    April 25, 2026

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    April 25, 2026

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    April 24, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    YANGA, AZAM FC USO KWA USO KUSAKA FAINALI YA MUUNGANO

    SIMBA YASHIKA NAFASI YA 19 DUNIANI, IPO LEVO ZA MADRID

    HILI HAPA DAU LA KUMPATA COLE PALMER

    TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMAMOSI TAREHE 25.4.2025

    PRESHA YA KUUKOSA UBINGWA YATAWALA REAL MADRID

    TAREHE PAMOJA NA UWANJA AMBAO DABI YA KARIAKOO ITAPIGWA

    SIMBA SC YAWINDA MAJIBU KWA MLANDAGE, SI KISASI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.