Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » BARKER AWAPA MZIGO MZITO MWALIMU, GUEYE NA OURA SIMBA
    KITAIFA

    BARKER AWAPA MZIGO MZITO MWALIMU, GUEYE NA OURA SIMBA

    ChikaoBy ChikaoApril 3, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KUELEKEA mchezo wa Mzizima Derby, Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker, ameweka wazi kuwa ana kazi kubwa ya kuiboresha safu ya ushambuliaji ya kikosi chake, akiwataka washambuliaji wake kuwa watulivu zaidi wanapofika katika eneo la umaliziaji.

    Barker aliyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa dakika 90 za mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam.

    Licha ya ushindi huo muhimu, kocha huyo alieleza kuridhishwa na kiwango cha jumla cha timu yake, lakini hakusita kubainisha mapungufu yaliyojitokeza, hususan kupoteza mipira mara kwa mara na kushindwa kutumia vyema nafasi walizozipata.

    Safu ya ushambuliaji ya Simba, inayoundwa na Selemani Mwalimu, Anicet Oura, Libasse Gueye pamoja na Neo Maema, sasa imepewa jukumu la kuhakikisha inakuwa makini zaidi mbele ya lango, hasa katika michezo ijayo yenye ushindani mkubwa.

    Barker amesema changamoto hiyo ilionekana zaidi katika kipindi cha kwanza, ambapo licha ya kutengeneza nafasi nyingi za kufunga, washambuliaji walikosa utulivu wa mwisho ulioweza kuzaa mabao zaidi.

    “Wachezaji wamepambana na kufanikisha kupata alama tatu, lakini bado nina kazi ya kurekebisha maeneo hayo. Kipindi cha kwanza tulitengeneza nafasi nyingi ambazo kwa utulivu zaidi tungeweza kufunga mabao manne au matano,” amesema Barker.

    Amesisitiza uwa ushindi huo ni chachu ya maandalizi ya michezo ijayo, huku akiahidi kuendelea kukinoa kikosi chake ili kuhakikisha kinakuwa imara katika kila idara.

    Barker ameongeza kuwa baada ya mchezo huo, macho yao sasa yanaelekezwa kwenye pambano lijalo dhidi ya Azam FC, akisisitiza umuhimu wa kuibuka na ushindi ili kuendelea kujiweka kwenye nafasi nzuri katika mbio za ubingwa.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleSelemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae
    Next Article MBAPPE: NITACHEZEA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.