Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » BACCA ATUPA TAULO, AKIRI RUSHINE NI BALAA
    KITAIFA

    BACCA ATUPA TAULO, AKIRI RUSHINE NI BALAA

    ChikaoBy ChikaoApril 3, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KIWANGO kinachooneshwa na beki wa Simba, Rushine De Reuck, kimeendelea kuvuta hisia za mashabiki na wadau wa soka ndani na nje ya uwanja, huku hata wapinzani wakikiri wazi ubora wake.

    Safari hii, pongezi hizo zimetolewa na beki wa Yanga, Ibrahim Hamad maarufu kama Bacca, ambaye ameonesha kuvutiwa na namna nyota huyo anavyotekeleza majukumu yake uwanjani.

    Bacca amesema tangu kuwasili kwa Rushine ndani ya kikosi cha Simba, safu ya ulinzi imepata mabadiliko makubwa yanayoonekana katika michezo ya hivi karibuni, akibainisha kuwa uwepo wake umeongeza uimara na kuleta hali ya kujiamini kwa wachezaji wenzake.

    Amesisitiza kuwa si jambo la kawaida kwa mchezaji kuingia kwenye ligi mpya na kuonesha kiwango cha juu kwa haraka kiasi hicho, hali inayomfanya Rushine kuwa miongoni mwa mabeki wanaoheshimika kwa sasa.

    “Naamini Rushine ameongeza kitu kipya kwenye ligi yetu. Ni beki bora sana na wote tumekuwa tukiona kazi yake uwanjani. Anastahili sifa zote kwa sababu anaonesha ubora mkubwa,” amesema Bacca.

    Mbali na uwezo wake wa kuzuia mashambulizi, Bacca ameongeza kuwa Rushine anachangia pia katika kujenga mashambulizi kutoka nyuma kwa utulivu mkubwa, jambo linaloifanya Simba kuwa na mfumo imara zaidi wa uchezaji.

    Amesema  ushindani uliopo kati ya Simba na Yanga unaendelea kupanda kutokana na uwepo wa wachezaji wa kiwango cha juu kama Rushine, hali inayosaidia kuinua hadhi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa ujumla.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleDURU LA PILI MOTO, DEPU ARUDI, YANGA YAANZA VITA RASMI
    Next Article Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    Related Posts

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    April 8, 2026

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    April 8, 2026

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    April 7, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    MPANZU NA FEI TOTO WAKUTANA USO KWA USO KWENYE VITA YA ASSIST

    IBENGE ATANGAZA VITA JUU YA KIKOSI CHA SIMBA

    MBAPPE: NITACHEZEA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.