Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » Refa Aliyeinyima Singida Penati Dhidi ya Simba Afungiwa Mizunguko Mitatu
    KITAIFA

    Refa Aliyeinyima Singida Penati Dhidi ya Simba Afungiwa Mizunguko Mitatu

    ChikaoBy ChikaoMarch 20, 202601 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Mwamuzi Katanga Hussein kutoka Tabora amefungiwa kuchezesha mechi kwa mizunguko mitatu (3) baada ya kubainika kushindwa kutafsiri ipasavyo sheria za mpira wa miguu.

    Adhabu hiyo inatokana na tukio la mchezo kati ya Singida Black Stars na Simba SC uliochezwa katika dimba la Uwanja wa Airtel Mtipa.

    Katika mchezo huo uliomalizika kwa Simba SC kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, mwamuzi huyo alishindwa kutoa penalti kwa Singida Black Stars licha ya tukio la wazi ambapo golikipa wa Simba, Djibrilla Kassali, alimfanyia madhambi mshambuliaji Joseph Guede ndani ya eneo la hatari.

    Kwa mujibu wa taarifa rasmi, uamuzi huo umetolewa na Tanzania Premier League Board (TPLB), kupitia Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, baada ya tathmini kuonesha kuwa mwamuzi alifanya makosa ya kiufundi yaliyokiuka sheria za mchezo.

    Mbali na adhabu hiyo, Singida Black Stars pia imetozwa faini ya shilingi milioni tano kutokana na meneja wao, Othmen Najjar, kushindwa kuzingatia kanuni za mavazi kwa maofisa wa timu wakati wa mchezo huo.

    Hatua hiyo inaonyesha msisitizo wa Tanzania Premier League Board katika kuhakikisha sheria na taratibu za ligi zinazingatiwa kikamilifu na wadau wote wa mchezo.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleShabiki wa Yanga Afungiwa Miezi 12 Kwa Uharibifu wa Mali
    Next Article AUDIO Hanstone Ft Nippi – Usijisumbue DOWNLOAD MP3

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.