Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » MO DEWJI AHOJI MAGEUZI SIMBA, GUMZO MTANDAONI
    KITAIFA

    MO DEWJI AHOJI MAGEUZI SIMBA, GUMZO MTANDAONI

    ChikaoBy ChikaoFebruary 11, 202602 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    MO DEWJI AHOJI MAGEUZI SIMBA, GUMZO MTANDAONI
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    WAKATI uongozi wa klabu ya Simba ukiendelea kusukuma mbele ajenda ya mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji, mwekezaji na Rais wa Heshima wa klabu hiyo, Mohammed Dewji (Mo Dewji), ameibua sintofahamu kubwa baada ya kuhoji hadharani hatua iliyofikiwa katika mchakato huo, akionekana kutoridhishwa na mwelekeo unaochukuliwa.

    Sintofahamu hiyo imejitokeza kufuatia Simba kusaini mikataba ya makubaliano na Mainstream Group pamoja na Nexus Pesa kwa ajili ya urejeshaji wa zoezi la usajili wa wanachama na utoaji wa kadi za uanachama kwa kuzingatia katiba ya klabu, kuanzia ngazi ya matawi hadi makao makuu.

    Hata hivyo, wakati uongozi ukieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mageuzi yanayolenga kuimarisha uendeshaji wa klabu, Mo Dewji kupitia mtandao wa kijamii ameonekana kuvuta breki ghafla kwa kuuliza swali moja lenye uzito mkubwa, “Transformation mmefikia wapi?”

    Swali hilo, lililoandikwa kwenye ukurasa rasmi wa Instagram wa Simba leo Februari 10, 2026, lilikuwa ni mchango wa Mo Dewji katika taarifa iliyokuwa ikimnukuu Mwenyekiti wa klabu, Murtaza Mangungu, kuhusu kurejeshwa kwa usajili wa wanachama,  hatua iliyotarajiwa kuleta umoja lakini badala yake imefungua mjadala mpana.

    Kauli hiyo ya Mo Dewji imezua tafsiri tofauti miongoni mwa Wanasimba, wengine wakiona kama ni ujumbe wa kuhoji uwazi wa mchakato wa mabadiliko, huku wengine wakitafsiri kama ishara ya kuwepo kwa tofauti za kimtazamo kati ya mwekezaji huyo na uongozi wa klabu.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleTanzania Yaiomba China Msaada Kukamilika Miundo Mbinu ya AFCON 2027
    Next Article PEDRO KILA KITU REHANI, YANGA KUPIGANIA ROBO FAINALI

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.