Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » Arsenal Warejea Kileleni EPL Baada ya Ushindi Mwembamba Dhidi ya Everton
    KIMATAIFA

    Arsenal Warejea Kileleni EPL Baada ya Ushindi Mwembamba Dhidi ya Everton

    ChikaoBy ChikaoDecember 21, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Arsenal
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Arsenal wamerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England (EPL) kufuatia ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Everton katika dimba la Hill Dickinson, jijini Liverpool.

    Bao pekee la mchezo lilifungwa dakika ya 27 na Viktor Gyökeres kwa mkwaju wa penalti, bao lililotosha kuwapa The Gunners alama zote tatu muhimu.

    Kwa ushindi huo, Arsenal wamefikisha pointi 39 baada ya michezo 17, wakipanda hadi nafasi ya kwanza, alama mbili mbele ya Manchester City, ambao wameshuka hadi nafasi ya pili baada ya kukaa kileleni kwa muda mfupi.

    Everton walijitahidi kusaka bao la kusawazisha hasa kipindi cha pili, lakini safu ya ulinzi ya Arsenal iliendelea kuwa imara na kuhakikisha wageni wanaondoka na ushindi.

    Matokeo hayo yanaendeleza ushindani mkali kileleni mwa EPL huku mbio za ubingwa zikizidi kuchangamka.

    FT: Everton 0-1 Arsenal
    ⚽ 27’ Gyökeres (P)

    Arsenal FC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleHii Hapa Ratiba ya AFCON 2025
    Next Article Jumapili ya Soka Ulaya: Mechi Kubwa Bundesliga, Serie A na LaLiga

    Related Posts

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    April 17, 2026

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    April 16, 2026

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    April 7, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.