Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SINTOFAHAMU YAIBUKA KWA KOCHA MPYA WA SIMBA
    KITAIFA

    SINTOFAHAMU YAIBUKA KWA KOCHA MPYA WA SIMBA

    ChikaoBy ChikaoOctober 4, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    kocha mpya wa simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Klabu ya Simba Sc imemtambulisha kocha Dimitri Pantev kama meneja wa timu hiyo huku vyanzo vikieleza kocha mkuu wa Wekundu hao wa Msimbazi atakuwa Selemani Matola kwenye makaratasi ingawa Pandev atakuwa kiongozi na mtendaji mbele ya benchi la ufundi wakati wa michezo.

    Kocha huyo raia wa Bulgaria ana leseni ya UEFA A hivyo hana vigezo ya kusimama kama Kocha Mkuu kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika kwa kuwa anatakiwa kuwa na leseni za CAF A au CAF Pro Licence au UEFA Pro Licence kwa Kocha anayetumia leseni kutoka Mashirikisho mengine nje na CAF.

    Hali hii ilishawahi kutokea huko Azam Fc wakati Yousuf Dabo ambaye alikuwa anatambulika kama Kocha Mkuu alikosa leseni stahiki hivyo Azam Fc wakamteua Bruno Ferry Kocha Mkuu kwenye makaratasi huku Dabo ambaye alitajwa kama Kocha Msaidizi akionekana kama ndiye Kocha kiongozi na mtendaji mbele ya benchi la ufundi wakati wa michezo.

    Hata hivyo, taarifa ya Simba Sc imemtambulisha Pantev kama Meneja wa timu hiyo huku sintofahamu ikizuka juu ya nani hasa atakuwa Kocha Mkuu wa klabu hiyo na ni ipi nafasi ya ya Selemani Matola ambaye awali alitambulishwa kama Kocha wa muda (caretaker) baada ya kuondoka kwa Fadlu Davids?

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleKOCHA ANAETAJWA KUTUA SIMBA AAGWA NA KLABU YAKE RASMI
    Next Article “MUDA WOWOTE CEO WA SIMBA ATAJIUZULU, AMECHOKA KUENDESHWA” – ALLY KAMWE

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.