Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป GERSON MSIGWA AKANUSHA TAARIFA ZA UWANJA WA MKAPA KUFUNGIWA MIEZI 6
    KITAIFA

    GERSON MSIGWA AKANUSHA TAARIFA ZA UWANJA WA MKAPA KUFUNGIWA MIEZI 6

    ChikaoBy ChikaoOctober 5, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    msigwa
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Msemaji Mkuu wa Serikali, Mhe. Gerson Msigwa, amekanusha taarifa zinazosambaa kuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa umefungwa kwa miezi sita.

    “ACHENI KUPOTOSHA.

    Hatujatangaza kuufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa miezi 6 kama baadhi ya watu wanavyopotosha.

    Tumekaa na TFF na pia timu za Yanga na Simba zilioomba kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya mechi za ligi na kufanya tathmini ya uharibifu wa sehemu ya kuchezea (pitch) ya uwanja wa Benjamin Mkapa baada ya mechi mfululizo zilizopita za Kimataifa na za ligi. Tumekubaliana kuwa Yanga na Simba watafute viwanja vingine kwa ajili ya michezo ya ligi na uwanja wa Benjamin Mkapa ubaki kwa ajili ya mechi za Kimataifa, Timu ya Taifa na Dabi mpaka hapo tutakapofanya ukarabati mkubwa wa pitch.

    Wale wanaohoji Bilioni 31 zilizotumika kukarabati uwanja, ni hivi ukarabati huo haukuhusisha ukarabati wa pitch. Ulihusisha kuboresha jengo, kuweka mifumo mipya ya umeme na taa, maji, vyoo, njia ya kukimbilia, kuweka viti vyote 62,000, kuweka viyoyozi, mfumo wa sauti, ubao wa matangazo, mabenchi ya ufundi, magoli, kupaka rangi na mfumo wa sauti.

    Walioingia Uwanja wa Benjamin Mkapa nambieni kipi hakijafanyika kati ya hivyo?

    Pia ni vizuri pia kujua kuwa uwanja mkubwa kama Benjamin Mkapa kila unapotumika ni lazima ufuatiwe na marekebisho kwa sababu hakuna tukio linaloweza kufanya bila kusababisha uharibifu. Na hii sio kwa uwanja huu tu ni viwanja vyote Dunia, na ukarabati wake unahitaji utaalamu na sio kubondabonda.

    TAZAMENI PICHA ZA HALI YA UWANJA BAADA YA MECHI 6 MFULULIZO. Na hapo Singida na Azam hawakutumia.

    Kumbukeni kulingana na maelekezo ya kitaalamu ya matumizi sahihi ya uwanja wa nyasi halisi (natural grass) uwanja unapaswa kutumika mara mbili au tatu tu kwa wiki. Hope tumeelewana”.Ameandika Msigwa kupitia Instagram yake.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleTAKWIMU YA ROMAIN FOLZ KATIKA MECHI 6 AKIWA YANGA
    Next Article HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 6, 2025

    Related Posts

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    April 8, 2026

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    April 8, 2026

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    April 7, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    MPANZU NA FEI TOTO WAKUTANA USO KWA USO KWENYE VITA YA ASSIST

    IBENGE ATANGAZA VITA JUU YA KIKOSI CHA SIMBA

    MBAPPE: NITACHEZEA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.