Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » SIMBA IPO KAMILI KUWAVAA GABORONE LEO, MECHI YA KIMATAIFA
    KITAIFA

    SIMBA IPO KAMILI KUWAVAA GABORONE LEO, MECHI YA KIMATAIFA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 20, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    simba
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    SEPTEMBA 20 2025 ni Gaborone United vs Simba SC mchezo wa hatua ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo wababe hawa watakuwa katika dakika 90 za kusaka ushindi kabla ya mchezo wa pili utakaotoa mshindi wa jumla atakayekwenda hatua inayofuata.

    Fadlu Davids, Kocha Mkuu wa Simba SC amesema wanachohitaji ni ushindi ili kutimiza malengo ya kwenda hatua ya makundi.

    “Ili upate nafasi ya kwenda hatua ya makundi ambacho kinahitajika ni ushindi. Mechi zote iwe ugenini na nyumbani ni muhimu kushinda na sisi tumejiandaa kufanya hivyo.

    “Timu yangu imecheza mechi mbili zenye uzito mkubwa Simba Day na Ngao ya Jamii kwa hiyo imetuongezea ubora.

    “Hata hivyo namuheshimu sana kocha wa timu pinzani naiheshimu hii timu kwa sababu wao ni mabingwa,”.

    Simba SC itakuwa Uwanja wa Francistown ikiwa ni hatua ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika saa 2:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

    Miongoni mwa wachezaji waliopo Botswana ni Ellie Mpanzu, Mousa Camara, Kibu Dennis, Joshua Mutale na Wilson Nangu. Miongoni mwa wachezaji ambao wataukosa mchezo wa leo ni Hamza ambaye ni beki alipata maumivu kwenye mchezo dhidi ya Yanga SC na Mohamed ambaye huyu alisajiliwa akiwa na majeraha bado hajawa imara.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleYANGA YAPATA USHINDI WAKE WA KWANZA KIMATAIFA
    Next Article HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 21 2025

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.