Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป NEYMAR AACHIWA URITHI WA TRIL 2+ NA MTU ASIEMJUA
    KIMATAIFA

    NEYMAR AACHIWA URITHI WA TRIL 2+ NA MTU ASIEMJUA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 5, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Nchini Brazil kumeibuka simulizi ya kushtua baada ya bilionea mwenye umri wa miaka 31 kutoka jimbo la Rio Grande do Sul kuamua kumwachia nyota wa soka Neymar Jr mali zake zote, licha ya wawili hao kutokuwa na uhusiano wowote wa karibu au hata kukutana ana kwa ana.

    Kwa taarifa za vyombo vya habari vya kimataifa, kijana huyo tajiri hakuwa na mke wala watoto, na mwezi Juni 2025 aliandika wosia rasmi katika ofisi ya serikali ukiwa na mashahidi. Katika hati hiyo alielekeza majumba, kampuni na vitega uchumi vyake vyote vyenye thamani ya zaidi ya dola bilioni 1 (takribani shilingi trilioni 2.5 za Kitanzania) viende kwa Neymar pekee.

    Sababu ya uamuzi huo imetajwa kuwa ni heshima na imani yake kwa utu wa Neymar, hususan unyenyekevu na ukaribu wake na baba yake, kitu kilichomvutia sana bilionea huyo.

    Kwa sasa, urithi huo mkubwa unasubiri kupitishwa kisheria na mahakama za Brazil kabla ya kuhamishiwa rasmi kwa staa huyo wa Paris Saint-Germain na timu ya taifa ya Brazil.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleMBEBA MIKOBA YA AZIZ KI YANGA SC BALAA LAKE ZITO
    Next Article TAIFA STARS KUINGIA KAZINI LEO

    Related Posts

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    April 17, 2026

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    April 16, 2026

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    April 7, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.