Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » MOURINHO ATANGAZA VITA KALI DHIDI YA CHELSEA LEO
    KIMATAIFA

    MOURINHO ATANGAZA VITA KALI DHIDI YA CHELSEA LEO

    ChikaoBy ChikaoSeptember 30, 202501 Min Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    Kocha Mkuu wa Benfica ya Ureno, Jose Mourinho, anarejea leo kwenye dimba la Stamford Bridge, uwanja wenye historia kubwa katika maisha yake ya soka. Safari hii anarejea kama mpinzani, akiiongoza Benfica kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mabingwa wa dunia, Chelsea. Mourinho alitangazwa kuwa kocha mkuu wa Benfica wiki iliyopita na leo anakabiliwa na mtihani wake mkubwa wa kwanza akiwa na timu hiyo mpya.

    Akizungumza kuelekea mchezo huo, Mourinho alisema anajihisi kama yupo nyumbani lakini sasa anawakilisha Benfica na lengo lake ni moja tu — kushinda. “Najihisi kama niko nyumbani, lakini ndani ya dakika 90 sitafikiria nilikotoka. Mimi si ‘The Blues’ tena, mimi ni mwekundu wa Benfica na nataka kushinda,” alisema.

    Mourinho aliwahi kuinoa Chelsea katika vipindi viwili tofauti (2004–2007 na 2013–2015) na kuandika historia kwa kutwaa mataji makubwa ikiwemo ubingwa wa Ligi Kuu England mara tatu, Kombe la FA mara moja, Kombe la Ligi mara tatu na Ngao ya Jamii mara moja. Kurejea kwake Stamford Bridge leo ni tukio la kihistoria linaloleta kumbukumbu nyingi, huku dunia ya soka ikisubiri kuona kama “The Special One” ataandika ukurasa mwingine wa kukumbukwa.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleWAJUE WAPINZANI WA SIMBA MECHI INAYOFUATA CAF
    Next Article TETESI: NABI YUPO MBIONI KUIONA KLABU HII KUBWA NCHINI

    Related Posts

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    April 7, 2026

    MBAPPE: NITACHEZEA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

    April 4, 2026

    TETESI: TIMU YA MESSI YAMFUKUZIA BERNARDO SILVA

    March 25, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    SIMBA YAANZA USAJILI NA MIPANGO YA UWANJA MPYA BUNJU

    SURE BOY HATIMAE AOMBA KUSEPA YANGA

    HATIMAE MIGUU IMEANZA KUMSALITI CHAMA

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    MPANZU NA FEI TOTO WAKUTANA USO KWA USO KWENYE VITA YA ASSIST

    IBENGE ATANGAZA VITA JUU YA KIKOSI CHA SIMBA

    MBAPPE: NITACHEZEA TIMU YA TAIFA YA CAMEROON

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.