Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home ยป JEAN AHOUA AINGIA KWENYE MTIHANI MWINGINE SIMBA
    KITAIFA

    JEAN AHOUA AINGIA KWENYE MTIHANI MWINGINE SIMBA

    ChikaoBy ChikaoSeptember 15, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    JEAN Ahoua kiungo mshambuliaji namba moja wa Simba SC kwenye mtihani mwingine ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids itakuwa Septemba 16 2025.

    Ahoua ni namba moja kwenye utengenezaji mipango ndani ya kikosi hicho, msimu wa 2024/25 alitengeneza jumla ya pasi 9 za mabao.

    Mbali na kutengeneza pasi hizo 9 za mabao alifunga jumla ya mabao 16 akiwa ni mshambuliaji namba moja kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara inayodhaminiwa na NBC.

    Katika pasi na mabao aliyofunga alikwama kufunga mbele ya watani zao wa jadi Yanga SC na alikwama kutengeneza pasi mbele ya watani zake hao jambo ambalo linamfanya awe kwenye mtihani mwingine kujibu maswali aliyokwama msimu uliopita.

    Kazi inatarajiwa kuanza Septemba 16 2025 kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii ambapo wababe hawa wawili wanatarajiwa kukutana.

    Vita yake kubwa ilikuwa na mwamba Pacome ambaye ni kiungo mshambuliaji wa Yanga SC huyu aliwapa dozi Simba SC walipokutana kwenye mchezo wa funga kazi Uwanja wa Mkapa mzunguko wa pili baada ya kufunga bao moja na kutoa pasi ya bao wakati ubao uliposoma Yanga SC 2-0 Simba SC.

    Ni siku moja imebaki kwa watani hawa kukutana uwanjani huku kila mmoja akivutia kwake kuhusu kuanza vema kwa kutwaa taji la Ngao ya Jamii.

    Ikumbukwe kwamba kwenye mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia, Ahoua alianza kikosi cha kwanza na alifungua akaunti ya pasi za mabao alipompa Hamza dakika ya 7 na mwisho ubao wa Uwanja wa Mkapa Septemba 10 2025 ulisoma Simba SC 2-0 Gor Mahia.

    Simba SC
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleZIMBWE JR AFIKIRIA MAKUBWA YANGA SC
    Next Article YAMEBAKI MASAA KUELEKEA DABI YA KARIAKOO

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.