Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » KOCHA SIMBA SC FADLU DAVIDS AFICHUA HESABU KUELEKEA MSIMU MPYA
    KITAIFA

    KOCHA SIMBA SC FADLU DAVIDS AFICHUA HESABU KUELEKEA MSIMU MPYA

    ChikaoBy ChikaoAugust 7, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    KOCHA Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids amesema kuwa wamefanya maboresho makubwa kwenye kikosi kwa kupata saini za wachezaji ambao watakuwa na kazi kupambana kwenye mashindano ambayo watashiriki.

    Simba SC msimu wa 2024/25 ilishiriki Kombe la Shirikisho Afrika na kugotea hatua ya fainali ikiwa nafasi ya pili na bingwa alikuwa RS Berkane. Msimu wa 2025/26 Simba SC itapeperusha bendera kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Fadlu ameweka wazi kuwa watakuwa kwenye aina tofauti ya mashindano ambayo yanahitaji ushindani mkubwa na aina ya wachezaji waliopo watakuwa na kazi kupambania ushindi.

    “Unaona kuna wachezaji ambao wamesaini kwenye kikosi. Ni aina ya wachezaji wazuri ni saini nzuri ambazo zipo kwenye kikosi. Tutakuwa kwenye mashindano tofauti msimu huu ukiachana na ligi tutakuwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

    “Aina ya ushindani kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika ni tofauti na kwenye Kombe la Shirikisho Afrika hivyo muhimu ni kuwa imara na tayari kwa ajili ya ushindani kwenye mechi zetu ambazo tutacheza.

    “Kambi ambayo ipo kwa sasa ninaona tunaendelea vizuri kuna mechi ambazo tutacheza kwa ajili ya kuwa imara zaidi hivyo bado tuna muda wakufanya maandalizi zaidi.”

    Miongoni mwa wachezaji wapya ambao wamesajiliwa Simba SC ni Jonathan Sowah mshambuliaji aliyekuwa Singida Black Stars, Abrahm Morice, beki wa kushoto Anthony Mligo aliyekuwa ndani ya Namungo FC.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleYANGA SC NA HAIER FAMILIA, BILIONI 3.3 KUVUNWA
    Next Article MAXIMO NA HESABU KUBWA NDANI YA KMC, MASHINE MPYA YATAMBULISHWA

    Related Posts

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    April 19, 2026

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    April 19, 2026

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    April 19, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.