Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    SOKALEO
    • HOME
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • TETESI ZA SOKA
    • MAGAZETI YA LEO
    • FORUM
    • BOXING
    SOKALEO
    Home » CHELSEA FC MABINGWA FIFA CLUB WORLD CUP 2025 MBELE YA PSG
    KIMATAIFA

    CHELSEA FC MABINGWA FIFA CLUB WORLD CUP 2025 MBELE YA PSG

    ChikaoBy ChikaoJuly 14, 202502 Mins Read
    Share Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Share
    WhatsApp Facebook Telegram Twitter Pinterest Email

    FIFA Club World Cup 2025 mashindano haya yalianza kurindima Juni 14 na kugota mwisho Julai 13 2025 ambapo ni Chelsea kutoka England ilitwaa taji hilo mbele ya PSG kwa ushindi wa mabao 3-0 ni usiku wa kuamkia Juni 14 fainali ilichezwa.

    Ni mabao ya Cole Palmer ambaye alifunga mabao mawili dakika 22 na 30 mbele ya PSG na bao moja likifungwa na Joao Pedro dakika 43. Kazi iliisha kabla ya mapumziko mbele ya Rais wa Marekani Donald Trump ambaye alikuwa sambamba na Rais wa FIFA Gianni Infantino.

    Enzo Maresca aliwapa mbinu wachezaji wa Chelsea kupata ushindi mbele ya PSG. Mashabiki wengi hawakutarajia hili ila imetokea. Mbinu za Luis Enrigue Kocha Mkuu wa PSG zilikwama.

    Luis Enrique alipata makasiriko baada ya kupoteza mchezo huo. Ilionekana walikuwa kwenye mzozo na Joan Pedro wa Chelsea.

    Kulikuwa na makundi 8 katika mashindano na viwanja 12 vilitumika kwa ajili ya mechi 63 ambazo zilichezwa nchini Marekani ambao walikuwa wenyeji wa mashindano haya makubwa.

    Fainali ilichezwa Uwanja wa MetLife na mchezo wa ufunguzi ulichezwa Uwanja wa Miami’s Hard Rock.

    Taji la FIFA Club World Cup ambalo ni jipya ubunifu wake umepita kwa wataalamu kutoka FIFA wakishirikiana na Global Luxury Jeweller Tiffany & CO.

    Shughuli za ushindani ilikuwa ni kutoka timu 32 ambazo zilishiriki mashindano hayo makubwa na Bara la Afrika pia kulikuwa na timu ambazo zilishiriki.

    Afrika ni timu nne ambapo tatu zilipatikana kutoka CAF Champions League na moja kutokana na raking yao, Asia timu 4, Europe 12, America ya Kati timu 4, Oceania timu moja, America ya Kusini timu 6 na timu mwenyeji alitoa timu moja.

    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Email
    Previous ArticleWANAOACHWA NA KUBAKI SIMBA NA YANGA HAWA HAPA
    Next Article PACOME KUONGEZA MKATABA YANGA SC

    Related Posts

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    April 17, 2026

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    April 16, 2026

    AFCON EAST AFRICA TAREHE YATANGAZWA

    April 7, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    TETESI: YANGA YAHAMISHIA MAJESHI KWA WINGA WA SINGIDA

    KIBABAGE NA KANTE KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA NAMUNGO

    KAMWE AZUNGUMZA JUU YA YANGA KUMSAJILI “SELEMANI MWALIMU”

    REFA ATUMIA SIMU KAMA VAR

    SINGIDA BLACK STARS WAZIPIGA MKWARA SIMBA, YANGA NA AZAM FC

    BERNARDO AAGWA NA MAN CITY RASMI

    WANA SIMBA WASIFEDHESHWE, TUNAJUA NAMNA YA KUPUNGUZA POINTI

    © 2026 SOKALEO TANZANIA | All Rights Are Reserved

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.